Swali: Je, inafaa kulipa siku nilizokula za Ramadhaan katika kumi la mwisho la Sha´baan au kabla yake kwa nisba ya mwanamke?
Jibu: Hapana vibaya kwa nisba ya mwanamke na mwanamme wote wawili. Inafaa kuchelewesha ulipaji mpaka katika Sha´baan. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anahaa) alikuwa akichelewesha mpaka Sha´baan. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ
“… hivyo basi akamilishe idadi katika siku nyinginezo.”[1]
Hakutenga wakati maalum na wala hakusema kuwa ni lazima kuharakisha. Ikafahamisha kuwa jambo ni lenye wasaa. Inasihi akilipa siku za Ramadhaan katika Shawwaal, Dhul-Qa´adah, Dhul-Hijjaah, Muharram, Swafar na miezi mingine.
[1] 02:184
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/10551/حكم-تاخير-قضاء-رمضان-الى-شعبان
- Imechapishwa: 27/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)