Swali: Je, inajuzu kuapa kwa asiyekuwa Allaah?
Jibu: Haijuzu kuapa kwa asiyekuwa Allaah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Tanabahini! Allaah anakukatazeni kuapa kwa baba zenu. Mwenye kutaka kuapa basi naape kwa Allaah au anyamaze.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Katika upokezi wa Abu Daawuud na an-Nasaa´iy kupitia kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) Marfuu´ah imekuja:
“Msiape kwa baba zenu wala mama zenu na wala msiape kwa Allaah isipokuwa muwe ni wakweli.”
Abu Daawuud na at-Tirmidhiy wamepokea kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah amekufuru na kufanya shirki.”
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (1/231)
- Imechapishwa: 24/08/2020
Swali: Je, inajuzu kuapa kwa asiyekuwa Allaah?
Jibu: Haijuzu kuapa kwa asiyekuwa Allaah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Tanabahini! Allaah anakukatazeni kuapa kwa baba zenu. Mwenye kutaka kuapa basi naape kwa Allaah au anyamaze.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Katika upokezi wa Abu Daawuud na an-Nasaa´iy kupitia kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) Marfuu´ah imekuja:
“Msiape kwa baba zenu wala mama zenu na wala msiape kwa Allaah isipokuwa muwe ni wakweli.”
Abu Daawuud na at-Tirmidhiy wamepokea kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah amekufuru na kufanya shirki.”
Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (1/231)
Imechapishwa: 24/08/2020
https://firqatunnajia.com/inafaa-kuapa-kwa-asiyekuwa-allaah/