Swali: Imesuniwa kufanya safu tatu ikiwa idadi ya wenye kuswali ni ndogo?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Hakuna mtu yeyote muislamu anayekufa na akaswaliwa na wanaume ishirini wasiomshirikisha Allaah na chochote isipokuwa Allaah atamsamehe kwao.”[1]
Kadhalika imesihi kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Hakuna muislamu anayekufa akaswaliwa na safu tatu za waislamu isipokuwa atasamehewa.”[2]
Kuna wanachuoni waliosema kuwa imependekezwa kuwafanya wakawa safu tatu hata kama katika kila moja kutakuwa watu wawili wawili.
Wengine wamesema makusudio ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa hilo ni wingi na wakatumia dalili ya Hadiyth ya pili inayosema:
“… wanaume arubaini… “
Hili ndilo lililo karibu [zaidi na usawa].
Kujengea juu ya hili naonelea kuwa bora zaidi ikamilizwe safu ya kwanza baada ya nyingine. Kukipatikana wingi lengo litakuwa limefikiwa.
[1] Muslim (59) na (948)
[2] Ahmad (04/79), Abuu Daawuud (3166) na at-Tirmidhiy (1028).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/107-108)
- Imechapishwa: 07/09/2021
Swali: Imesuniwa kufanya safu tatu ikiwa idadi ya wenye kuswali ni ndogo?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Hakuna mtu yeyote muislamu anayekufa na akaswaliwa na wanaume ishirini wasiomshirikisha Allaah na chochote isipokuwa Allaah atamsamehe kwao.”[1]
Kadhalika imesihi kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Hakuna muislamu anayekufa akaswaliwa na safu tatu za waislamu isipokuwa atasamehewa.”[2]
Kuna wanachuoni waliosema kuwa imependekezwa kuwafanya wakawa safu tatu hata kama katika kila moja kutakuwa watu wawili wawili.
Wengine wamesema makusudio ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa hilo ni wingi na wakatumia dalili ya Hadiyth ya pili inayosema:
“… wanaume arubaini… ”
Hili ndilo lililo karibu [zaidi na usawa].
Kujengea juu ya hili naonelea kuwa bora zaidi ikamilizwe safu ya kwanza baada ya nyingine. Kukipatikana wingi lengo litakuwa limefikiwa.
[1] Muslim (59) na (948)
[2] Ahmad (04/79), Abuu Daawuud (3166) na at-Tirmidhiy (1028).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/107-108)
Imechapishwa: 07/09/2021
https://firqatunnajia.com/imesuniwa-kufanya-safu-tatu-ikiwa-idadi-ya-wenye-kuswali-ni-ndogo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)