Swali: Baada ya Fajr na Maghrib imamu anatakiwa kubaki hali ya kuelekea Qiblah mpaka alete Tahliyl?
Jibu: Hapana, ni kosa. Sunnah ni yeye kuwaelekea waswaliji anaposema:
واللهم أنت السلام ومنك السلام تباركت يا ذا الجلال والإكرام
“Ee Allaah! Wewe ndiye as-Salaam, amani inatoka Kwako, umebarikika, Ee Mwenye utukufu na ukarimu.”
Awageukia maamuma. Hii ndio Sunnah.
Swali: Je, kuna makatazo ya kuelekea Qiblah?
Jibu: Hapana, hichi ndicho kilikuwa kitendo cha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Swalini kama mlivyoniona ninaswali.”
Alikuwa akileta Maghfirah mara tatu husema:
واللهم أنت السلام ومنك السلام تباركت يا ذا الجلال والإكرام
“Ee Allaah! Wewe ndiye as-Salaam, amani inatoka Kwako, umebarikika, Ee Mwenye utukufu na ukarimu.”
kisha anawageukia watu. Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) aliyesema:
“Mtume alikuwa akigeuka wakati anapomaliza kusema:
واللهم أنت السلام ومنك السلام تباركت يا ذا الجلال والإكرام
“Ee Allaah! Wewe ndiye as-Salaam, amani inatoka Kwako, umebarikika, Ee Mwenye utukufu na ukarimu.”
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22137/هل-يهلل-الامام-الى-القبلة-في-الفجر-والمغرب
- Imechapishwa: 31/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket