Sa´iyd bin Mansuur bin Shu´bah, Haafidhw, Imaam, Shaykh wa msikiti Mtakatifu, Abu ´Uthmaan al-Khuraasaaniy al-Marwaziy na inasemekana at-Twalaqaaniy, kisha al-Balkhiy, kisha al-Makkiy. Mtunzi wa ”as-Sunan”.
Baadhi ya aliowasikia Khuraasaan, Hijaaz, ´Iraaq, Misri, Shaam na Kurdistan ni pamoja na Maalik bin Anas, al-Layth bin Sa´d, Hushaym, Ismaa´iyl bin ´Ayyaash, al-Fudhwayl bin ´Iyaadhw, Sufyaan bin ´Uyaynah na wengineo.
Alikuwa mkweli, mwaminifu na chombo cha elimu.
Miongoni mwa waliopokea kutoka kwake ni pamoja na Ahmad bin Hanbal, Abu Thawr al-Kalbiy, Abu Muhammad ad-Daarimiy, Abu Bakr al-Athram, Abu Daawuud, Muslim, Muhammad bin Yahyaa adh-Dhuhaliy, Abu Haatim ar-Raaziy na wengineo.
Salamah bin Shabiyb amesema:
”Nilimtaja Sa´iyd bin Mansuur mbele ya Ahmad bin Hanbal ambapo akamsifu na akamuadhimisha.”
Abu Haatim ar-Raaziy amesema:
“Ni mwaminifu na ni miongoni mwa watu mairi imara waliokusanya na wakatunga.”
Harb al-Kirmaaniy amesema:
“Sa´iyd bin Mansuur alitusomea karibu Hadiyth 100.000 kutoka kichwani mwake.”
Nasema: Alikuwa takriban na miaka 80 wakati alipofariki Makkah Ramadhaan mwaka 227.
Harb bin Ismaa´iyl amesema:
”Ametunga vitabu na akavifanya kwa kiwango kikubwa.”
Ya´quub al-Fasaawiy amesema:
“Alikuwa anapoona kwenye kitabu chake kosa, basi hajirejei.”
Nasema: Linganisha haya na rafiki yake Imaam Yahyaa bin Yahyaa al-Khuraasaaniy ambaye alikuwa akiiacha Hadiyth nzima pindi anapotilia mashaka herufi yake.
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (10/586-595)
- Imechapishwa: 29/09/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)