Kusujudu kwa kuanza magoti ndio bora zaidi kisha ndio mtu afuatishe mikono, paji la uso na pua. Mtu asianze kusujudu kwa mikono. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza hilo pale aliposema:
“Mmoja wenu anapoenda katika Sujuud, asishuke kama anavoshuka ngamia.”[1]
Ngamia huanza kwenda chini kwa mikono kama jinsi imevyoshuhudiwa. Kila anayemuona ngamia anapoenda chini ameona kuwa anatanguliza mikono kwanza. Hivyo usitangulizwe mikono. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza hilo. Binadamu kujifananisha na wanyama, khaswa katika swalah, ni jambo lisilotakikana.
[1]Abu Daawuud (840).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (01/395)
- Imechapishwa: 31/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)