Swali: Kuna katika wanachuoni wenye kuonelea kuwa inafaa kuwasomea Qur-aan maiti na kwamba thawabu zake zinawafikia. Ni upi usawa katika hayo?
Jibu: Usawa ni kwamba haziwafikii. Shaykh Taqiyy-ud-Diyn amethibitisha kuwa hazimfikii pasi na mzozo. Kumsomea Qur-aan thawabu hazimfikii. Isitoshe haijuzu kuchukua malipo kwa jambo hilo. Kwa kuwa haikupokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yenye kuthibitisha kwamba thawabu zinamfikia. Yaliyothibiti ni kujikurubisha kwa swadaqah, hajj na ´umrah. Haya yanamfikia na yanawanufaisha wale maiti. Ama masuala ya kumsomea hakuna dalili juu ya hilo. Kuhusu kuwaombea du´aa kunawafaa. Kumethibiti dalili juu ya hilo na maafikiano ya waislamu. ´Ibaadah zimejengwa juu ya Qur-aan na Sunnah peke yake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 43
- Imechapishwa: 16/11/2016
Swali: Kuna katika wanachuoni wenye kuonelea kuwa inafaa kuwasomea Qur-aan maiti na kwamba thawabu zake zinawafikia. Ni upi usawa katika hayo?
Jibu: Usawa ni kwamba haziwafikii. Shaykh Taqiyy-ud-Diyn amethibitisha kuwa hazimfikii pasi na mzozo. Kumsomea Qur-aan thawabu hazimfikii. Isitoshe haijuzu kuchukua malipo kwa jambo hilo. Kwa kuwa haikupokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yenye kuthibitisha kwamba thawabu zinamfikia. Yaliyothibiti ni kujikurubisha kwa swadaqah, hajj na ´umrah. Haya yanamfikia na yanawanufaisha wale maiti. Ama masuala ya kumsomea hakuna dalili juu ya hilo. Kuhusu kuwaombea du´aa kunawafaa. Kumethibiti dalili juu ya hilo na maafikiano ya waislamu. ´Ibaadah zimejengwa juu ya Qur-aan na Sunnah peke yake.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 43
Imechapishwa: 16/11/2016
https://firqatunnajia.com/ibn-baaz-kuhusu-thawabu-za-kisomo-cha-qur-aan-kumfikia-maiti/