Nchi hii – kwa himdi za Allaah – haifanya kitu ambacho kinapelekea kufanya uasi dhidi yake. Watu pekee ambao wanaona kufaa kufanya uasi dhidi ya nchi kwa sababu ya madhambi ni Khawaarij ambao wanawakufurisha waislamu kwa sababu ya madhambi. Wanawapiga vita waislamu na kuwasalimisha waabudia mizimu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Wanatoka katika dini kama ambavo mshale unatoka katika upinde wake.”

Amesema tena:

“Wapigeni vita popote mtapokutana nao. Kwani mwenye kuwaua ana ujira mkubwa mbele ya Allaah siku ya Qiyaamah.”

Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim na kuna Hadiyth nyingi juu yao na zinazotambulika.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu Fataawaa wa Maqaalaat Mutanawwi´ah (4/91)
  • Imechapishwa: 01/04/2024