Ibn Baaz kuhusu mwanamke kuvaa viatu vya visigino virefu

Swali: Ni ipi hukumu ya Uislamu kuhusu kuvaa viatu vya visigino virefu?

Jibu: Dogo liwezalo kusemwa ni kuchukiza, kwa sababu zifuatazo:

1 – Vinamuonyesha mwanamke kuwa ni mrefu ilihali sio mrefu.

2 – Vinamtia katika khatari mwanamke kuanguka.

3 – Vina madhara kwa afya, kama walivyothibitisha hivo madaktari.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1879/حكم-لبس-الكعب-العالي
  • Imechapishwa: 10/10/2024