Swali: Kuna mtu ameingia msikitini na akamkuta imamu yuko katika Tahiyyaat katika Rak´ah ya mwisho na safu imejaa. Je, akae chini na kuswali peke yake?
Jibu: Aswali peke yake.
Swali: Je, apange safu kwenye safu?
Jibu: Hapana, aswali peke yake.
Swali: Nakusudia kwamba asijiunge pamoja na wengine?
Jibu: Hapana. Asijiunge pamoja na mkusanyiko muda wa kuwa hakupata nafasi.
Swali: Endapo ataswali peke yake katika safu atalazimika kuirudia swalah yake?
Jibu: Ndio. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwamrisha kuirudia swalah yake aliyeswali peke yake.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22237/ما-يفعل-من-دخل-المسجد-والصفوف-مكتملة
- Imechapishwa: 15/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)