Swali: Ni ipi hukumu ya kuyatembelea makaburi kufanya maalum siku ya ijumaa?
Jibu: Ni jambo lisilokuwa na msingi. Lililowekwa katika Shari´ah ni yule mwenye kuyatembelea makaburi ayatembelee wakati wowote itapokuwa sahali. Ni mamoja ikawa usiku au mchana. Kuhusu kuyatembelea siku maalum au usiku maalum ni Bid´ah isiyokuwa na msingi wowote. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atayezusha katika amri yetu hii yasiyokuwemo yatarudishwa.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
“Atakayefanya kitendo kisichoafikiana na amri yetu kitarudishwa.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.binbaz.org.sa/fatawa/2718
- Imechapishwa: 15/10/2016
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket