Swali: Je, kuna uthibitisho sahihi kuhusu swalah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuswali Rak´ah nne kabla ya Dhuhr bila kutoa salamu? Hadiyth isemayo:
”Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”?
ni Swahiyh? Vipi zinaoanishwa?
Jibu: Swalah ya kuswali Rak´ah nne mfululizo bila kutoa salamu ina udhaifu. Haikuthibiti kutokana na ninavyojua. Sunnah ni yeye kuswali kila baada ya Rak´ah mbili:
”Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”?
Hadiyth hii ni Swahiyh. Imekuja katika Hadiyth Swahiyh ya Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa):
”Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika swalah zake za sunnah akitoa salamu kila baada ya Rak´ah mbili. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiswali usiku Rak´ah kumi na akitoa salamu kila baada ya Rak´ah mbili kisha alikuwa akihitimisha kwa Rak´ah moja ya Witr.”
Hata hivyo inajuzu kuunganisha Rak´ah kwa Witr, kama vile kuswali Rak´ah tano mfululizo, tatu au saba bila kutoa salamu katikati, kama ilivyopokelewa kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Lakini haifai kwa mtu kuswali swalah ya kujitolea Rak´ah nne au sita au nane mfululizo bila kutoa salamu kila baada ya Rak´ah mbili. Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sunnah. Sunnah ni kutoa salamu baada ya kila Rak´ah mbili.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25133/هل-صح-صلاة-النبي-اربعا-قبل-الظهر-دون-فصل
- Imechapishwa: 05/02/2025
Swali: Je, kuna uthibitisho sahihi kuhusu swalah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuswali Rak´ah nne kabla ya Dhuhr bila kutoa salamu? Hadiyth isemayo:
”Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”?
ni Swahiyh? Vipi zinaoanishwa?
Jibu: Swalah ya kuswali Rak´ah nne mfululizo bila kutoa salamu ina udhaifu. Haikuthibiti kutokana na ninavyojua. Sunnah ni yeye kuswali kila baada ya Rak´ah mbili:
”Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”?
Hadiyth hii ni Swahiyh. Imekuja katika Hadiyth Swahiyh ya Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa):
”Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika swalah zake za sunnah akitoa salamu kila baada ya Rak´ah mbili. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiswali usiku Rak´ah kumi na akitoa salamu kila baada ya Rak´ah mbili kisha alikuwa akihitimisha kwa Rak´ah moja ya Witr.”
Hata hivyo inajuzu kuunganisha Rak´ah kwa Witr, kama vile kuswali Rak´ah tano mfululizo, tatu au saba bila kutoa salamu katikati, kama ilivyopokelewa kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Lakini haifai kwa mtu kuswali swalah ya kujitolea Rak´ah nne au sita au nane mfululizo bila kutoa salamu kila baada ya Rak´ah mbili. Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sunnah. Sunnah ni kutoa salamu baada ya kila Rak´ah mbili.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25133/هل-صح-صلاة-النبي-اربعا-قبل-الظهر-دون-فصل
Imechapishwa: 05/02/2025
https://firqatunnajia.com/ibn-baaz-kuhusu-kuswali-sunnah-rakah-nne-kwa-tasliym-moja/