Swali: Kuna mwanamke ni mtumzima sana na anaswali. Lakini hata hivyo anasema kuwa hajui zaidi ya kusema “at-Tahiyyaatu lillaahi, was-Swalawaatu wat-Twayyibaat” tu. Ni ipi hukumu ya hilo na Swalah yake inasihi au hapana?
Jibu: Ikiwa hajui at-Tahiyyaat isipokuwa maneno haya mane:
التحيات لله، و الصلوات و الطيبات
“Maadhimisho, swalah na mazuri yote yanamstahikia Allaah.”
yale yaliyomshinda yanamkatikia [hayamuwajibikii]. Allaah (Ta´ala) amesema:
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا
“Allaah hakalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya uwezo wake.” (02:286)
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Basi mcheni Allaah muwezavyo” (64:16)
Hatujui badala ya at-Tahiyyaat.
Kuhusu al-Faatihah mtu ikimshinda tunamwambia asome kitu kingine katika Qur-aan kwa kadiri ya al-Faatihah. Ikiwa hajui kitu chochote katika Qur-aan tunamwambia alete Tasbiyh, Tahliyl na Takbiyr kwa kiasi cha al-Faatihah kisha arukuu. Ama kuhusu Tashahhud haina badala. Ikiwa hajui jengine zaidi ya haya maneno mane itakuwa imemkatikia kutokana na maneno Yake (Ta´ala):
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Basi mcheni Allaah muwezavyo” (64:16)
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kanda “Liqaa´aatu Ramadhwaaniyyah”, sehemu ya 07
- Imechapishwa: 23/09/2020
Swali: Kuna mwanamke ni mtumzima sana na anaswali. Lakini hata hivyo anasema kuwa hajui zaidi ya kusema “at-Tahiyyaatu lillaahi, was-Swalawaatu wat-Twayyibaat” tu. Ni ipi hukumu ya hilo na Swalah yake inasihi au hapana?
Jibu: Ikiwa hajui at-Tahiyyaat isipokuwa maneno haya mane:
التحيات لله، و الصلوات و الطيبات
“Maadhimisho, swalah na mazuri yote yanamstahikia Allaah.”
yale yaliyomshinda yanamkatikia [hayamuwajibikii]. Allaah (Ta´ala) amesema:
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا
“Allaah hakalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya uwezo wake.” (02:286)
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Basi mcheni Allaah muwezavyo” (64:16)
Hatujui badala ya at-Tahiyyaat.
Kuhusu al-Faatihah mtu ikimshinda tunamwambia asome kitu kingine katika Qur-aan kwa kadiri ya al-Faatihah. Ikiwa hajui kitu chochote katika Qur-aan tunamwambia alete Tasbiyh, Tahliyl na Takbiyr kwa kiasi cha al-Faatihah kisha arukuu. Ama kuhusu Tashahhud haina badala. Ikiwa hajui jengine zaidi ya haya maneno mane itakuwa imemkatikia kutokana na maneno Yake (Ta´ala):
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Basi mcheni Allaah muwezavyo” (64:16)
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kanda “Liqaa´aatu Ramadhwaaniyyah”, sehemu ya 07
Imechapishwa: 23/09/2020
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-swalah-ambayo-mtu-anasoma-at-tahiyyaat-nusu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)