Swali: Je, inajuzu kwa mwenye kudai elimu kuwatolea mawaidha watu na kuwaelekeza na kukusanyika kwenye jeneza na kushirikiana na watu katika Bid´ah zao ili ya kuwatolea mawaidha na kuwanasihi kama jinsi anavyodai?
Jibu: Kushiriki katika Bid´ah kwa njia ya kunyamazia na kuridhia, haijuzu. Ama akienda sehemu ya Bid´ah ili kuwakumbusha na kutahadharisha kisha akawaacha pasina kushirikiana nao, hakuna neno. Akienda sehemu ya Bid´ah ili kuwatahadharisha dhidi ya Bid´ah – kwa kutumia fursa hii ya kukusanyika kwao – hili halina neno. Ama kushirikiana nao katika kusherehekea kwao na kudai kuwa anawatahadharisha, hapana. Huku sio kukataza. Awakataze na kuwatahadharisha na ajiweke mbali na kushirikiana nao katika Bid´ah. Hili ndilo la wajibu kwa kila mwenye elimu pale atapowatahadharisha watu kutokana na Bid´ah na kuwakataza Bid´ah wazifanyazo na atengane nao na wala asiwe pamoja nao na kushirikiana nao.
Swali: Wala asile nao hata maulidini?
Jibu: Asile kwenye maulidi. Kinyume chake awatahadharishe na kujitenga nao na awakataze.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=12822
- Imechapishwa: 03/05/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)