Swali: Unapendekeza kwa mwanafunzi ahifadhi Zaad-ul-Mustaqni´ au ´Umdat-ul-Fiqh?
Jibu: Haihusiani na kuhifadhi. Kuhifadhi sio kujifunza hata kama utahifadhi al-Mughni´. Huku sio kujifunza. Inahusiana na kwamba ukipata mwalimu anayeweza kukufunza na kukushereheshea kitabu, kila siku ukawa unahifadhi sehemu yake na akakushereheshea nayo. Kwa msemo mwingine ukakusanya kati ya kuhifadhi na kujifunza. Hili ni jambo zuri. Lakini kukaa tu na kuhifadhi sio kujifunza hata kama ungehifadhi dunia nzima. Hii ni ghururi tu. Huenda ukapatwa na ghururi ya kujiona uko mwanachuoni ilihali uko mjinga ingawa umehifadhi. Elimu sio kuhifadhi. Elimu ni ule uelewa:
“Yule ambaye Allaah anamtakia kheri humpa uelewa katika dini.”[1]
Uelewa ni kule kufahamu. Hili ndilo linatakikana. Ni wangapi wamehifadhi vitabu na hawaelewi kitu! Ukimuuliza kitu kidogo tu hawezi kukujibu.
[1] al-Bukhaariy (71).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (6) http://alfawzan.af.org.sa/node/14379
- Imechapishwa: 02/12/2016
Swali: Unapendekeza kwa mwanafunzi ahifadhi Zaad-ul-Mustaqni´ au ´Umdat-ul-Fiqh?
Jibu: Haihusiani na kuhifadhi. Kuhifadhi sio kujifunza hata kama utahifadhi al-Mughni´. Huku sio kujifunza. Inahusiana na kwamba ukipata mwalimu anayeweza kukufunza na kukushereheshea kitabu, kila siku ukawa unahifadhi sehemu yake na akakushereheshea nayo. Kwa msemo mwingine ukakusanya kati ya kuhifadhi na kujifunza. Hili ni jambo zuri. Lakini kukaa tu na kuhifadhi sio kujifunza hata kama ungehifadhi dunia nzima. Hii ni ghururi tu. Huenda ukapatwa na ghururi ya kujiona uko mwanachuoni ilihali uko mjinga ingawa umehifadhi. Elimu sio kuhifadhi. Elimu ni ule uelewa:
“Yule ambaye Allaah anamtakia kheri humpa uelewa katika dini.”[1]
Uelewa ni kule kufahamu. Hili ndilo linatakikana. Ni wangapi wamehifadhi vitabu na hawaelewi kitu! Ukimuuliza kitu kidogo tu hawezi kukujibu.
[1] al-Bukhaariy (71).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (6) http://alfawzan.af.org.sa/node/14379
Imechapishwa: 02/12/2016
https://firqatunnajia.com/haihusiani-na-kuhifadhi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)