Swali: Ni ipi hukumu kwa mfungaji kutumia dawa za kuingiza machoni, masikioni na puani?

Jibu: Kwa kuepuka mashaka ale, kwa sababu amehalalishiwa kula:

فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ

“Basi atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu au yuko safarini, hivyo basi akamilishe idadi katika siku nyinginezo.”[1]

Ikiwa ni mgonjwa na anahitaji matibabu basi tunamshauri ale na alipe baadaye. Hapa ni pale ambapo madaktari wamemwandikia kufanya matibabu mchana wa Ramadhaan. Vinginevyo hakuna kinachomfunguza isipokuwa kile kinachoshuka kooni. Mara nyingi anayetia wanja machoni huenda akahisi ladha yake kooni mwake. Kwa ajili hiyo tunamshauri kuepuka kitendo hicho.

[1] 02:184

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 79
  • Imechapishwa: 17/03/2024