Swali: Je, inafaa kwa mtu kuiacha Qur-aan wazi bila kuifunga pale anapomaliza kusoma kwa kuzingatia kwamba hasomi ndani yake?

Jibu: Ni kwa nini anaiacha wazi? Asiiache wazi. Aifunge. Kwa sababu kufanya hivo ni kukihifadhi zaidi Kitabu cha Allaah kwa njia ya kwamba vumbi wala kitu kingine kisiingie ndani yake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (40)
  • Imechapishwa: 18/05/2023