Swali: Je, mfungaji ambaye Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amehimiza kumfunguza ni yule mfungaji ambaye ni masikini, mgeni nchini au ni yule ambaye tunamwalika katika futari nyumbani kwetu kama mgeni katika ndugu na jamaa? Je, tunapata thawabu kwa kuwakaribisha futari wafungaji ambao tunawaalika mwaliko maalum ndani ya Ramadhaan?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba amesema:
“Yeyote atakayemfuturisha mfungaji basi anapata ujira mfano wake, ingawa hakupungui chochote katika ule ujira wa mfungaji.”
Ameipokea at-Tirmdihiy.
Makusudio ya mfungaji hapa ni mfungaji katika waislamu na khaswa ambaye anastahiki kupewa swadaqah kwa kulishwa kama mfano wa fakiri, masikini na msafiri. Maana hii ni mfano wa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yeyote atakayeandaa vita katika njia ya Allaah, basi amepigana vita.”
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh
Bakr Abu Zayd
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (09/34) nr. (17790)
- Imechapishwa: 24/04/2022
Swali: Je, mfungaji ambaye Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amehimiza kumfunguza ni yule mfungaji ambaye ni masikini, mgeni nchini au ni yule ambaye tunamwalika katika futari nyumbani kwetu kama mgeni katika ndugu na jamaa? Je, tunapata thawabu kwa kuwakaribisha futari wafungaji ambao tunawaalika mwaliko maalum ndani ya Ramadhaan?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba amesema:
“Yeyote atakayemfuturisha mfungaji basi anapata ujira mfano wake, ingawa hakupungui chochote katika ule ujira wa mfungaji.”
Ameipokea at-Tirmdihiy.
Makusudio ya mfungaji hapa ni mfungaji katika waislamu na khaswa ambaye anastahiki kupewa swadaqah kwa kulishwa kama mfano wa fakiri, masikini na msafiri. Maana hii ni mfano wa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yeyote atakayeandaa vita katika njia ya Allaah, basi amepigana vita.”
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh
Bakr Abu Zayd
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (09/34) nr. (17790)
Imechapishwa: 24/04/2022
https://firqatunnajia.com/fadhilah-za-kumfuturisha-mfungaji-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)