Swali: Ni ipi hukumu ya kuomba du´aa katika sehemu ya Multazam na kushikilia pazia ya Ka´bah?
Jibu: Kuomba du´aa katika Multazam hakuna tatizo. Jambo hili limefanywa na baadhi ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum). Imepokewa pia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alilifanya, ingawa kuna udhaifu katika kusihi kwake. Lakini kwa kuwa limefanywa na baadhi ya Maswahabah. Kusimama pale kati ya nguzo na mlango wa Ka´bah na kuomba du´aa ni jambo linalokubalika. Kuna matarajio ya kuitikiwa du´aa.
Ama kuhusu kushikilia pazia ya Ka´bah hatujui dalili yoyote ya Kishari´ah inayothibitisha hilo. Jambo hili halina msingi. Kinachojulikana katika Sunnah ni kile alichokifanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa ndani ya Ka´bah; aliweka kifua chake na mikono yake katika ukuta wa ndani na akamwomba Mola wake na akaleta Takbiyr. Imepokewa hivyo na Usaamah bin Zayd na Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhum) kwamba alizunguka ndani ya Ka´bah, akaleta Takbiyr na kuomba du´aa. Aidha imepokelewa kutoka kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kupitia masimulizi ya Bilaal kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali Rak´ah mbili ndani ya Ka´bah. Hayo ndiyo yaliyothibiti. Lakini kutoka nje ya Ka´bah, hakuna dalili inayothibitisha kushikilia pazia, isipokuwa upande wa Multazam ambapo aliomba du´aa kunajuzu.
Akiomba du´aa katika sehemu yoyote ya Haram hakuna tatizo. Lakini kushikilia pazia ya Ka´bah kwa dhana ya baraka, hilo halina msingi. Hatujui msingi wowote wa hilo.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1106/حكم-الدعاء-في-الملتزم-والتشبث-باستار-الكعبة
- Imechapishwa: 25/01/2026
Swali: Ni ipi hukumu ya kuomba du´aa katika sehemu ya Multazam na kushikilia pazia ya Ka´bah?
Jibu: Kuomba du´aa katika Multazam hakuna tatizo. Jambo hili limefanywa na baadhi ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum). Imepokewa pia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alilifanya, ingawa kuna udhaifu katika kusihi kwake. Lakini kwa kuwa limefanywa na baadhi ya Maswahabah. Kusimama pale kati ya nguzo na mlango wa Ka´bah na kuomba du´aa ni jambo linalokubalika. Kuna matarajio ya kuitikiwa du´aa.
Ama kuhusu kushikilia pazia ya Ka´bah hatujui dalili yoyote ya Kishari´ah inayothibitisha hilo. Jambo hili halina msingi. Kinachojulikana katika Sunnah ni kile alichokifanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa ndani ya Ka´bah; aliweka kifua chake na mikono yake katika ukuta wa ndani na akamwomba Mola wake na akaleta Takbiyr. Imepokewa hivyo na Usaamah bin Zayd na Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhum) kwamba alizunguka ndani ya Ka´bah, akaleta Takbiyr na kuomba du´aa. Aidha imepokelewa kutoka kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kupitia masimulizi ya Bilaal kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali Rak´ah mbili ndani ya Ka´bah. Hayo ndiyo yaliyothibiti. Lakini kutoka nje ya Ka´bah, hakuna dalili inayothibitisha kushikilia pazia, isipokuwa upande wa Multazam ambapo aliomba du´aa kunajuzu.
Akiomba du´aa katika sehemu yoyote ya Haram hakuna tatizo. Lakini kushikilia pazia ya Ka´bah kwa dhana ya baraka, hilo halina msingi. Hatujui msingi wowote wa hilo.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1106/حكم-الدعاء-في-الملتزم-والتشبث-باستار-الكعبة
Imechapishwa: 25/01/2026
https://firqatunnajia.com/duaa-sehemu-ya-multazam/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket