Swali: Hadiyth ya Salamah bin Akwa´ ya yule bwana aliyekula mbele ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa kutumia mkono wa kushoto ambapo akamwambia: ”Kula kwa mkono wa kulia.” Bwana yule akajibu kuwa hawezi. Akamwambia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): ”Hutoweza. Hakuna kichomzuia isipokuwa kufanya kiburi.” Je, hapa kunachumwa faida ya kufaa kumuombea du´aa mbaya muislamu anapoenda kinyume na amri ya Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?
Jibu: Kinachodhihiri katika Hadiyth ni kufaa itapojulikana kuwa amefanya jeuri. Lakini kusamehe ndio bora zaidi. Kumsamehe na kumuombea du´aa nduguyo ndio bora zaidi kama ilivyopokelewa katika maandiko mengine.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22348/ما-حكم-الدعاء-على-المسلم-اذا-خالف-الشرع
- Imechapishwa: 17/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)