Swali: Je, mtu anapata dhambi za wanaomfuata hata baada ya kutubu ikiwa alikuwa mpotofu kisha akaongoka?
Jibu: Kunatarajiwa kwake kusalimika – Allaah akitaka. Akitubu, basi – Allaah akitaka – kunatarajiwa kwake kusalimika. Kwa sababu tawbah inafuta madhambi ya kabla yake. Hata hivyo ni lazima kwake kubainisha kujirejea kwake.
Swali: Wako waliosema kuwa anapata dhambi za wanaomfuata hata baada ya kutubu kutokana na Hadiyth ya mwana wa Aadam ambaye alitubu na juu yake anabeba mzigo wa madhambi wa wanaomfuata.
Jibu: Hainidhihirikii. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kutubu juu ya dhambi ni kama hana dhambi yoyote.”
Tawbah inafuta yaliyo kabla yake. Mtoto wa Aadam hatujui kama alitubu au hakutubu? Je, wewe una khabari yoyote kwamba alitubia?
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22975/هل-يلحق-المفسد-بعد-توبته-وزر-من-تبعه
- Imechapishwa: 27/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)