Swali: Kuna wanaosema kuwa pindi ninapomwita walii na kusema:
“Ee fulani! Niponye!”
Nasema hivo kwa mafumbo. Ninachokusudia ni:
“Ee fulani! Niombee kwa Allaah aniponye!”
Jibu: Kwa nini basi useme: “Niponye!”. Badala yake sema: “Nitibu!” iwapo ni tabibu. Kwa nini useme: “Niponye!”. Tabibu anatibu na wala haponyi. Anachofanya yeye ni kutoa dawa tu na wala haponyi. Kuponya kunatoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Dawa ni sababu tu miongoni mwa sababu zingine. Usisemi tamko: “Niponye!” kumwambia kiumbe.
Swali: Tamko “Ee fulani! Niponye!” linazingatiwa kuwa ni shirki kubwa inayomtoa mtu katika Uislamu?
Jibu: Kwa hali yoyote ni kosa. Lakini ikiwa ana imani kuwa anaponya ndio inakuwa ni kumshirikisha Allaah. Ikiwa hana imani inahesabika ni kosa ambalo mtu anatakiwa kujiepusha nalo.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Furqaan (14) http://alfawzan.af.org.sa/node/2057
- Imechapishwa: 23/04/2017
Swali: Kuna wanaosema kuwa pindi ninapomwita walii na kusema:
“Ee fulani! Niponye!”
Nasema hivo kwa mafumbo. Ninachokusudia ni:
“Ee fulani! Niombee kwa Allaah aniponye!”
Jibu: Kwa nini basi useme: “Niponye!”. Badala yake sema: “Nitibu!” iwapo ni tabibu. Kwa nini useme: “Niponye!”. Tabibu anatibu na wala haponyi. Anachofanya yeye ni kutoa dawa tu na wala haponyi. Kuponya kunatoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Dawa ni sababu tu miongoni mwa sababu zingine. Usisemi tamko: “Niponye!” kumwambia kiumbe.
Swali: Tamko “Ee fulani! Niponye!” linazingatiwa kuwa ni shirki kubwa inayomtoa mtu katika Uislamu?
Jibu: Kwa hali yoyote ni kosa. Lakini ikiwa ana imani kuwa anaponya ndio inakuwa ni kumshirikisha Allaah. Ikiwa hana imani inahesabika ni kosa ambalo mtu anatakiwa kujiepusha nalo.
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Furqaan (14) http://alfawzan.af.org.sa/node/2057
Imechapishwa: 23/04/2017
https://firqatunnajia.com/daktari-anatibu-na-wala-haponyi/