Swali: Je, dada wa mke wangu kubaki nyumbani kwangu kwa masiku mengi na wavulana wangu bado ni wadogo na pengine wakati mwingine mama yao akatoka nyumbani inazingatiwa kuwa ni faragha ilioharamishwa?

Jibu: Ikiwa kuna wavulana ambao wameshafikia umri wa kuweza kupambanua mambo, haihesabiki kuwa ni kuwa faragha kwa uwepo wao. Vilevile ikiwa kutoka kwake ni kwa muda mrefu, kama kwa mfano wanawake waalimu ambao wanatoka na kwenda kufundisha, au wanatoka na kusafiri ili kwenda kufundisha kwa kuwa masomo yako mbali, au wanafundisha nje ya mji ulio mbali anaenda kwa masaa, haifai kufanya hivi. Lakini ikiwa kutoka kwake ni kwa muda mfupi na baadaye anarudi, wakati huohuo pamoja na kuwepo mtu nyumbani ambaye itahesabika hakukaa naye faragha, hakuna neno.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (38) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-2-4_1.mp3
  • Imechapishwa: 20/08/2020