Swali: Je, ziada inayosema ´na baraka Zake` (وبركاته) katika Tasliym imesihi?
Jibu: Imepokelewa katika Hadiyth hii. Haafidhw [Ibn Hajar] ametaja katika “Buluugh-ul-Maraam” ya kwamba ni sahihi. Lakini kikosi cha wanazuoni wengine wamesema kuwa kinapingana na zilizo Swahiyh. Kwa hivyo bora ni kusema tu:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na baraka za Allaah ziwe juu yenu.”
Kama inavofanywa hii leo. Hivo ndivo ilivyothibiti katika “as-Swahiyh” ya Muslim kupitia kwa Samurah ambaye amesimulia kwamba:
“Walikuwa wanaposalimia ndani ya swalah husema:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na baraka za Allaah ziwe juu yenu.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22983/هل-زيادة-وبركاته-في-التسليم-من-الصلاة-صحيحة
- Imechapishwa: 06/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)