Wakati wa swalah ya ´iyd unaanza pale linapochomoza jua kiasi cha mkuki. Huo ndio wakati ambao Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali ndani yake. Wakati wake unaendelea mpaka pale ambapo jua linapinduka.
´Iyd ikija kutambulika baada ya kuwa jua limeshapinduka, basi watu wataswali kesho hali ya kuilipa. Abu ´Umayr bin Anas amesema:
“Ulifichikana kwetu mwezi mwandamo wa Shawwaal tukaamka asubuhi hali ya kuwa tumefunga. Akaja mpandaji [farasi] mwishoni mwa mchana ambapo wakashuhudia kuwa waliona mwezi mwandamo wakati wa jana. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha wafungue siku yao na kesho watoke kwa ajili ya ´iyd yao.”
Ameipokea Ahmad, Abu Daawuud, ad-Daaraqutwniy ambaye amiefanya kuwa nzuri. Pia imesahihishwa na jopo la mahufadhi.
Ingelikuwa swalah ya ´iyd inaswaliwa baada ya kuwa limekwishapondoka, basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asingeichelewesha mpaka kesho.
Jengine ni kwa sababu kilichosuniwa katika swalah ya ´iyd ni mkusanyiko wa watu wote. Kwa hivyo ni lazima itanguliwe na wakati ambao watu wataweza kujiandaa kwa ajili yake.
Imependekezwa kutanguliza swalah ya ´Iy-ul-Adhwhaa na kuchelewesha swalah ya ´Iyd-ul-Fitwr. ash-Shaafi´iy amepokea upokezi ambao katika cheni ya wapokezi kuna Swahabah anayekosekana: “Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwandikia barua ´Amr bin Hamz:
“Iharakishe [swalah ya] al-Adhwhaa, ucheleweshe [swalah ya] al-Fitwr na muwakumbushe watu. Fanyeni wakati wa kuchinja uwe mpana kwa kuitanguliza swalah katika [´iyd] al-Adhwhaa. Fanyeni wakati wa kutoa Zakaat-ul-Fitwr kabla ya kuanza kuswali Swalat-ul-Fitwr.”
Imependekezwa kula baadhi ya tende kabla ya kutoka kwenda kuswali swalah ya ´Iyd-ul-Fitwr na mtu asile katika ´Iyd-ul-Adhwhaa mpaka kwanza kuswaliwe. Buraydah amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa hatoki siku ya ´Iyd-ul-Fitwr mpaka ale na wala hali siku ya ´Iyd-ul-Adhwhaa mpaka aswali kwanza.”
Ameipokea Ahmad na wengineo.
Shaykh Taqiyy-ud-Diyn amesema:
“Wakati Allaah alipotanguliza swalah kabla ya kuchinja pale aliposema:
فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ
”Basi swali kwa ajili ya Mola wako na [pia ukichinja] na chinja [kwa ajili Yake]!”[1]
na akatanguliza kuswali kabla ya kutoa zakaah pale aliposema:
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّىٰ
“Hakika amefaulu ambaye amejitakasa na akataja jina la Mola wake na akaswali.”[2]
ikawa imependekezwa kutanguliza swadaqah kabla ya kuswali katika ´Iyd-ul-Fitwr na kwamba kunachinja kunakuwa baada ya kuswali katika ´Iyd-ul-Adhwhaa.”
Imependekezwa kutoka mapema kwenda kuswali ´iyd ili apate kuwa karibu na imamu na pia mut apate fadhilah za kusubiri swalah na hivyo thawabu zake ziwe nyingi.
Imependekezwa kwa muislamu kujipamba kwa ajili ya kuswali ´iyd kwa kuvaa nguo yake nzuri kabisa. Jaabir amesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa na juba akilivaa siku katika ´iyd mbili na siku ya ijumaa.”
Ameipokea Ibn Khuzaymah katika “as-Swahiyh” yake.
Pia al-Bayhaqiy amepokea kwa cheni ya wapokezi nzuri kwamba Ibn ´Umar alikuwa akivaa katika ´iyd mbili nguo yake nzuri kabisa.
[1] 108:02
[2] 87:14-15
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mulakhaswsw-ul-Fiqh (01/269-271)
- Imechapishwa: 30/07/2020
Wakati wa swalah ya ´iyd unaanza pale linapochomoza jua kiasi cha mkuki. Huo ndio wakati ambao Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali ndani yake. Wakati wake unaendelea mpaka pale ambapo jua linapinduka.
´Iyd ikija kutambulika baada ya kuwa jua limeshapinduka, basi watu wataswali kesho hali ya kuilipa. Abu ´Umayr bin Anas amesema:
“Ulifichikana kwetu mwezi mwandamo wa Shawwaal tukaamka asubuhi hali ya kuwa tumefunga. Akaja mpandaji [farasi] mwishoni mwa mchana ambapo wakashuhudia kuwa waliona mwezi mwandamo wakati wa jana. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha wafungue siku yao na kesho watoke kwa ajili ya ´iyd yao.”
Ameipokea Ahmad, Abu Daawuud, ad-Daaraqutwniy ambaye amiefanya kuwa nzuri. Pia imesahihishwa na jopo la mahufadhi.
Ingelikuwa swalah ya ´iyd inaswaliwa baada ya kuwa limekwishapondoka, basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asingeichelewesha mpaka kesho.
Jengine ni kwa sababu kilichosuniwa katika swalah ya ´iyd ni mkusanyiko wa watu wote. Kwa hivyo ni lazima itanguliwe na wakati ambao watu wataweza kujiandaa kwa ajili yake.
Imependekezwa kutanguliza swalah ya ´Iy-ul-Adhwhaa na kuchelewesha swalah ya ´Iyd-ul-Fitwr. ash-Shaafi´iy amepokea upokezi ambao katika cheni ya wapokezi kuna Swahabah anayekosekana: “Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwandikia barua ´Amr bin Hamz:
“Iharakishe [swalah ya] al-Adhwhaa, ucheleweshe [swalah ya] al-Fitwr na muwakumbushe watu. Fanyeni wakati wa kuchinja uwe mpana kwa kuitanguliza swalah katika [´iyd] al-Adhwhaa. Fanyeni wakati wa kutoa Zakaat-ul-Fitwr kabla ya kuanza kuswali Swalat-ul-Fitwr.”
Imependekezwa kula baadhi ya tende kabla ya kutoka kwenda kuswali swalah ya ´Iyd-ul-Fitwr na mtu asile katika ´Iyd-ul-Adhwhaa mpaka kwanza kuswaliwe. Buraydah amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa hatoki siku ya ´Iyd-ul-Fitwr mpaka ale na wala hali siku ya ´Iyd-ul-Adhwhaa mpaka aswali kwanza.”
Ameipokea Ahmad na wengineo.
Shaykh Taqiyy-ud-Diyn amesema:
“Wakati Allaah alipotanguliza swalah kabla ya kuchinja pale aliposema:
فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ
”Basi swali kwa ajili ya Mola wako na [pia ukichinja] na chinja [kwa ajili Yake]!”[1]
na akatanguliza kuswali kabla ya kutoa zakaah pale aliposema:
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّىٰ
“Hakika amefaulu ambaye amejitakasa na akataja jina la Mola wake na akaswali.”[2]
ikawa imependekezwa kutanguliza swadaqah kabla ya kuswali katika ´Iyd-ul-Fitwr na kwamba kunachinja kunakuwa baada ya kuswali katika ´Iyd-ul-Adhwhaa.”
Imependekezwa kutoka mapema kwenda kuswali ´iyd ili apate kuwa karibu na imamu na pia mut apate fadhilah za kusubiri swalah na hivyo thawabu zake ziwe nyingi.
Imependekezwa kwa muislamu kujipamba kwa ajili ya kuswali ´iyd kwa kuvaa nguo yake nzuri kabisa. Jaabir amesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa na juba akilivaa siku katika ´iyd mbili na siku ya ijumaa.”
Ameipokea Ibn Khuzaymah katika “as-Swahiyh” yake.
Pia al-Bayhaqiy amepokea kwa cheni ya wapokezi nzuri kwamba Ibn ´Umar alikuwa akivaa katika ´iyd mbili nguo yake nzuri kabisa.
[1] 108:02
[2] 87:14-15
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mulakhaswsw-ul-Fiqh (01/269-271)
Imechapishwa: 30/07/2020
https://firqatunnajia.com/baadhi-ya-mambo-yaliyopendekezwa-katika-iyd/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)