´Iyd-ul-Adhwhaa inaizidi ´Iyd-ul-Fitwr kwa usuniwaji wa Takbiyr ndani yake. Nazo ni zile Takbiyr zilizowekwa katika Shari´ah baada ya kila swalah ya faradhi katika mkusanyiko. Imamu anatakiwa kuwageukia waswaliji kisha alete Takbiyr na wao pia walete Takbiyr. ad-Daaraqutwniy na Ibn Abiy Shaybah wamepokea kupitia kwa Jaabir ambaye amesimulia:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaposwali Fajr katika siku ya kufuata ya ´Arafah anasema:
“Allaahu Akbar… “
Takbiyr zilizofungamanishwa baada ya kila swalah kwa ambaye hayuko katika Ihraam zinaanza kuanzia swalah ya Fajr siku ya ´Arafah mpaka swalah ya ´Aswr ile siku ya mwisho ya kuchinja. Kwa ambaye yuko katika Ihraam Takbiyr zilizofungamanishwa kwake zinaanza kuanzia swalah ya Dhuhr ile siku ya kwanza ya kuchinja mpaka ´Aswr ile siku ya mwisho ya kuchinja. Kwa sababu kabla ya hapo yeye ameshughulishwa na kuleta Talbiyah.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mulakhaswsw-ul-Fiqh (01/279)
- Imechapishwa: 30/07/2020
´Iyd-ul-Adhwhaa inaizidi ´Iyd-ul-Fitwr kwa usuniwaji wa Takbiyr ndani yake. Nazo ni zile Takbiyr zilizowekwa katika Shari´ah baada ya kila swalah ya faradhi katika mkusanyiko. Imamu anatakiwa kuwageukia waswaliji kisha alete Takbiyr na wao pia walete Takbiyr. ad-Daaraqutwniy na Ibn Abiy Shaybah wamepokea kupitia kwa Jaabir ambaye amesimulia:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaposwali Fajr katika siku ya kufuata ya ´Arafah anasema:
“Allaahu Akbar… “
Takbiyr zilizofungamanishwa baada ya kila swalah kwa ambaye hayuko katika Ihraam zinaanza kuanzia swalah ya Fajr siku ya ´Arafah mpaka swalah ya ´Aswr ile siku ya mwisho ya kuchinja. Kwa ambaye yuko katika Ihraam Takbiyr zilizofungamanishwa kwake zinaanza kuanzia swalah ya Dhuhr ile siku ya kwanza ya kuchinja mpaka ´Aswr ile siku ya mwisho ya kuchinja. Kwa sababu kabla ya hapo yeye ameshughulishwa na kuleta Talbiyah.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mulakhaswsw-ul-Fiqh (01/279)
Imechapishwa: 30/07/2020
https://firqatunnajia.com/takbiyr-baada-ya-zile-swalah-tano-za-faradhi-misikitini/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)