2868- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Hakuna neno juu yako – si vyenginevyo ni baba na mtumwa wako tu.”
Ameipokea adh-Dhwiyaa´ katika ”al-Mukhtaarah” kupitia kwa Abu Daawuud, kutoka kwa Abu Jaamiy´ Saalim bin Diynaar, kutoka kwa Thaabit, kutoka kwa Anas ambaye amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuja kwa Faatwimah na mtumwa ambaye alikuwa amemzawadia. Faatwimah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuwa na kanzu ambayo, pindi anafunika kwayo kichwa chake basi haifiki miguuni mwake, na pindi anapofunika miguu yake, haifiki kichwani mwake. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipoona hali aliyomo akasema: ”Hakuna neno juu yako – si vyenginevyo ni baba na mtumwa wako tu.”
Cheni ya wapokezi ni Swahiyh.
Katika Hadiyth kuna dalili ya wazi kabisa kwamba inafaa kwa mwanamke kuonesha kichwa na miguu yake mbele ya baba yake na mtumwa wake. Ndani yake kuna Radd kwa Abul-A´laa al-Mawduudiy (Rahimahu Allaah) ambaye amesema waziwazi kwamba haitakiwi kwa mwanamke kuonesha uso na miguu yake mbele ya baba yake, ami yake, kaka yake, mtoto wake wa kiume mpaka wanawake mfano wake[1]!
[1] al-Hijaab, uk. 289-290
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (6/2/869)
- Imechapishwa: 21/07/2020
2868- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Hakuna neno juu yako – si vyenginevyo ni baba na mtumwa wako tu.”
Ameipokea adh-Dhwiyaa´ katika ”al-Mukhtaarah” kupitia kwa Abu Daawuud, kutoka kwa Abu Jaamiy´ Saalim bin Diynaar, kutoka kwa Thaabit, kutoka kwa Anas ambaye amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuja kwa Faatwimah na mtumwa ambaye alikuwa amemzawadia. Faatwimah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuwa na kanzu ambayo, pindi anafunika kwayo kichwa chake basi haifiki miguuni mwake, na pindi anapofunika miguu yake, haifiki kichwani mwake. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipoona hali aliyomo akasema: ”Hakuna neno juu yako – si vyenginevyo ni baba na mtumwa wako tu.”
Cheni ya wapokezi ni Swahiyh.
Katika Hadiyth kuna dalili ya wazi kabisa kwamba inafaa kwa mwanamke kuonesha kichwa na miguu yake mbele ya baba yake na mtumwa wake. Ndani yake kuna Radd kwa Abul-A´laa al-Mawduudiy (Rahimahu Allaah) ambaye amesema waziwazi kwamba haitakiwi kwa mwanamke kuonesha uso na miguu yake mbele ya baba yake, ami yake, kaka yake, mtoto wake wa kiume mpaka wanawake mfano wake[1]!
[1] al-Hijaab, uk. 289-290
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (6/2/869)
Imechapishwa: 21/07/2020
https://firqatunnajia.com/anayoweza-kudhihirisha-mwanamke-mbele-ya-baba-na-mtumwa-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)