Anayeweza kuhiji na hakuhiji

Swali 11: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Yeyote aliyeweza kufanya hajj na asihiji, basi afe akitaka myahudi au mnaswara.”[1]

Nini maana ya hilo?

Jibu: Hadiyth hii katika usahihi wake kuna mtazamo. Maana – ikiwa Hadiyth ni Swahiyh – ni kwamba akifa, basi kunakhofiwa kwamba atakuwa kafiri ama pamoja na mayahudi au pamoja na manaswara.

[1] at-Tirmidhiy amepokea mfano wake (812) na akasema:

”Hadiyth hii ni ngeni.”

Ni dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf-ul-Jaamiy´” (5860).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (21/23)
  • Imechapishwa: 08/05/2026