Swali: Anayepinga kupangusa juu ya soksi anakuwa mtu wa Bid´ah? Kwa nini wanachuoni wameingiza somo la kupangusa juu ya soksi katika milango ya ´Aqiydah?

Jibu: Wenye kuona kuwa haijuzu kupangusa juu ya soksi ni Shiy´ah Raafidhwah. Hawa ndio wanaona kuwa haijuzu kupangusa juu ya soksi. Maandiko yamepokelewa kwa njia nyingi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ni rukhusa na ni jambo limethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Pamoja na hivyo wanapinga hili.

Kuhusiana na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaona kuwa inajuzu kupangusa juu ya soksi kwa masharti yaliyotajwa. Hakuna anayepinga hili isipokuwa ni mtu wa Bid´ah au mtu mwenye kujifananisha na Shiy´ah.

Lililo la ajabu ni kwamba Shiy´ah wanaona kuwa haijuzu kupangusa juu ya soksi, pamoja na kuwa imethibiti kutoka kwa Mtume, lakini wao wanapangusa juu ya miguu yao. Ni mgongano aina gani huu ulio wa batili! Tunaomba Allaah Atukinge. Wanapangusa juu ya miguu na hawaoshi [mtu wenyewe].

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (46) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-4-27.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020