Amemjamii mke wake Ramadhaan ya kwanza bila ya kujua

Kutoka kwa Muhammad bin Ibraahiym kwenda kwa muheshimiwa X.

السلام عليكم ورحمة الله وبركاته

Nimefikiwa na barua yako ambayo ndani imejumuisha mwanaume ambaye amemjamii mke wake siku ya kwanza ya Ramadhaan na yeye hakuwa anajua kuwa siku hiyo ni Ramadhaan.

Jawabu ni kwamba madhehebu yanasema kuwa analazimika kulipa na kutoa kafara. Hata hivyo kuna maoni mengine yanayosema kuwa hatolazimika kutoa kafara, kwa sababu alikuwa mwenye kupewa udhuru na ndio chaguo la Taqiyy-ud-Diyn [Ibn Taymiyyah] na wengineo. Haya ya pili ndio maoni ya sawa – Allaah akitaka.

Muftiy wa Saudi Arabia

08/07/1384

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Ibraahiym Aalush-Shaykh
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (04/195)
  • Imechapishwa: 20/03/2024