Swali: Kuna mtu ameamka kutoka usingizini baada ya jua kuchomoza na bado hajaswali Fajr. Je, inafaa kwake kuichelewesha Fajr mpaka wakati wa kupondoka kwa jua?
Jibu: Hapana. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Yule mwenye kusahau swalah au akapitikiwa na usingizi, basi aiswali pale atakapoikumbuka. Haina kafara nyingine isipokuwa hiyo.”
Anapaswa kuharakisha kuiswali pasi na kujali ni wakati gani, hata kama ni katika wakati wa makatazo aiswali.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (39)
- Imechapishwa: 01/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)