Swali: Msichana wangu aliacha kufunga baadhi ya siku za Ramadhaan kwa sababu ya machovu. Je, analazimika kutoa swadaqah?

Jibu: Halazimiki kulipa swadaqah, kwa sababu Allaah (´Azza wa Jall) amesema:

فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ

“Basi atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu, au yuko safarini [akafunga baadhi ya siku], basi [akamilishe] idadi [ya siku anazotakiwa kufunga] katika siku nyinginezo.”[1]

Allaah hakutaja swadaqah yoyote.

[1] 02.184

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/384)
  • Imechapishwa: 26/04/2026