al-Haakim ameeleza kuwa amemsikia Ibn Khuzaymah akisema:
“Anashuka (Ta´ala) chini kila usiku katika mbingu ya chini na kusema:
”Kuna mwenye kuomba apewe? Kuna mwenye kuomba aitikiwe? Kuna mwenye kuomba msamaha asamehewe?”[1]
Anayedai kuwa kinachoshuka ni amri Yake amepotea. Anawazungumzisha waja Wake, bila kulifanyia namna:
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Si kama walivodai Jahmiyyah, kwamba ametawala. Allaah anawazumgisha waja Wake mwanzo na mwisho na anawakariria visa, amri na makatazo Yake. Ambaye atadai kinyume na hivo basi ni mpotevu na mzushi.”
[1] al-Bukhaariy (7494) na Muslim (758).
[2] 20:05
- Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (14/381)
- Imechapishwa: 20/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)