Imaam at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
“[Allaah] hahitajii kitu:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (42:11)
Hahitajii kitu miongoni mwa vitu. Neno “kitu” linahusiana na viumbe vyote. Hamuhitajii kiumbe yeyote kutokana na ukamilifu wa utajiri Wake. Maneno Yake:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye… “
Hii ni Radd kwa Mumaththilah na Mushabbihah. Maneno Yake:
وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.”
Hii ni Radd kwa Mu´attwilah ambao wanapinga majina na sifa za Allaah. Ni Aayah ilio na Radd kwa mapote mawili:
1- Mumaththilah.
2- Mushabbihah.
Mushabbihah wanamfananisha Allaah na viumbe Vyake na wanazipigia mfano sifa za Allaah na sifa za viumbe. Ni Radd vilevile kwa Mu´attwilah ambao wanakanusha majina na sifa za Allaah.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/96)
- Imechapishwa: 31/05/2020
Imaam at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
“[Allaah] hahitajii kitu:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (42:11)
Hahitajii kitu miongoni mwa vitu. Neno “kitu” linahusiana na viumbe vyote. Hamuhitajii kiumbe yeyote kutokana na ukamilifu wa utajiri Wake. Maneno Yake:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye… ”
Hii ni Radd kwa Mumaththilah na Mushabbihah. Maneno Yake:
وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.”
Hii ni Radd kwa Mu´attwilah ambao wanapinga majina na sifa za Allaah. Ni Aayah ilio na Radd kwa mapote mawili:
1- Mumaththilah.
2- Mushabbihah.
Mushabbihah wanamfananisha Allaah na viumbe Vyake na wanazipigia mfano sifa za Allaah na sifa za viumbe. Ni Radd vilevile kwa Mu´attwilah ambao wanakanusha majina na sifa za Allaah.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/96)
Imechapishwa: 31/05/2020
https://firqatunnajia.com/allaah-taala-hahitajii-kitu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)