al-Ikhwaan al-Muslimuun wamechukua kiapo katika dunia hii cha usikivu na uatiifu

Ndugu waliofilifika – al-Ikhwaan al-Muflisuun, yaani. al-Ikhwaan al-Muslimuun – na wengineo katika watu wanaofuata matamanio yao wanawafanya watu wale kiapo… Kiapo cha nini? Kiapo kuwaahidi usikivu na utiifu kwa dunia hii na pesa. Wamefanya hivo pamoja na kwamba hawako katika Jihaad wala katika kupigana vita na kufuru. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kufa na hana juu ya shingo yake bay´ah (hakula kiapo cha usikivu na utiifu kumpa mtawala wa Waislamu), basi amekufa kifo cha Jaahiliyyah.”

Kiongozi akiomba hilo, basi ni wajibu kwa wale Waislamu wanaoweza Indonesia na kwenginepo kumpa ahadi ya usikivu na utiifu. Wale wasioweza waagize bay´ah zao.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://muqbel.org/sounds.php?sound_id=29
  • Imechapishwa: 22/04/2015