al-Fawzaan kuhusu ujinga ni udhuru 2

Swali: Je, ni wanachuoni peke yao ndio wenye kufaa kuonelea kuwa waabudu makaburi kwa dhati yao ni makafiri au ni wajibu vilevile hata kwa watu wa kawaida?

Jibu: Wanachuoni wote, watu wa kawaida, wenye kuishi mjini na mabedui anayeabudu asiyekuwa Allaah ni mshirikina. Kusema kwamba umpe udhuru kwa kuwa ni mjinga… Allaah ndiye mwenye kujua zaidi. Ujinga una mipaka yake. Anaishi wapi? Je, anaishi mbali na Uislamu na wala hajui lolote? Katika hali hii huyu ni mjinga.

Lakini yule mwenye kuishi kati ya Waislamu, anakuja Misikitini na anasikia Qur-aan, Hadiyth na darsa – mpaka lini atakuwa mjinga? Je, ujinga wake utakatika siku ya Qiyaamah? Sio sahihi [kufikiria hivo]. Haijuzu kuwatafutia watu nyudhuru na kuchukulia mambo sahali namna hii. Haya ni madhehebu ya Murji-ah. Madhehebu ya Murji-ah yako njiani yanatujia hivi sasa kupitia watu wetu wenyewe. Ni juu yetu kuwa hange.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/nawaqid-18-08-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 11/04/2015