Swali: Kuna wanaowaita wavulana wao kwa jina la Luutw akifanya hivo kwa kukusudia kuwakumbusha watu fedheha ya tendo la liwati. Je, kitendo chake ni sahihi?
Jibu: Vipi? Anamwita Luutw kwa sababu ya kuwatahadharisha watu na liwati? Haya ni maoni ya ajabu. Amwite Luutw kwa sababu ni Nabii na si kwa sababu ya uliwati. Amwite kwa sababu ni jina la Nabii mtukufu. Luutw, Nuuh na Ibraahiym, haya ni majina ya Manabii (´alayhimus-Swalaatu was-Salaam).
Luutw (´alayhis-Salaam) aliitwa kwa jina hili kabla ya Allaah Kumtuma kwa kundi hili.
فَآمَنَ لَهُ لُوطٌ
“Basi Luutw akamwamini.” (29:26)
Hapa ni katika ardhi ya Iraaq. Kabla ya yeye kuhama kwenda katika ardhi ya Shaam alikuwa anaitwa Luutw tokea asli. Haina mnasaba wowote kwa kutumwa kwa wanaliwati. Lisiambatanishwe kati ya hili na hili.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (01) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1427-1-30.mp3
- Imechapishwa: 17/08/2020
Swali: Kuna wanaowaita wavulana wao kwa jina la Luutw akifanya hivo kwa kukusudia kuwakumbusha watu fedheha ya tendo la liwati. Je, kitendo chake ni sahihi?
Jibu: Vipi? Anamwita Luutw kwa sababu ya kuwatahadharisha watu na liwati? Haya ni maoni ya ajabu. Amwite Luutw kwa sababu ni Nabii na si kwa sababu ya uliwati. Amwite kwa sababu ni jina la Nabii mtukufu. Luutw, Nuuh na Ibraahiym, haya ni majina ya Manabii (´alayhimus-Swalaatu was-Salaam).
Luutw (´alayhis-Salaam) aliitwa kwa jina hili kabla ya Allaah Kumtuma kwa kundi hili.
فَآمَنَ لَهُ لُوطٌ
“Basi Luutw akamwamini.” (29:26)
Hapa ni katika ardhi ya Iraaq. Kabla ya yeye kuhama kwenda katika ardhi ya Shaam alikuwa anaitwa Luutw tokea asli. Haina mnasaba wowote kwa kutumwa kwa wanaliwati. Lisiambatanishwe kati ya hili na hili.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (01) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1427-1-30.mp3
Imechapishwa: 17/08/2020
https://firqatunnajia.com/al-fawzaan-kuhusu-kumpa-mtoto-jina-la-luutw/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)