Swali: Ni ipi adhabu ya mwanamke ambaye anamuasi mume wake katika mambo mema, anatangamana naye vibaya kwelikweli na anaomba talaka pasi na sababu? Je, inafaa kwake kwenda kwa familia yake mume wake akioa mwanamke mwingine juu yake?

Jibu: Kuna juu yake matishio makali. Amefanya dhambi kubwa:

“Mwanamke yeyote ambaye atamuomba mumewe talaka pasi na sababu basi ni haramu juu yake harufu ya Pepo.”

Namna hii imethibiti katika Hadiyth. Pia imepokelewa:

“Mwanamme akimwita mke wake ambapo akalala hali ya kuwa amemkasirikia, basi Malaika humlaani mpaka kupambazuke.”

Au matamshi kama hayo. Hata hivyo mwanamke ni mwenye kupewa udhuru ikiwa amefanya hivo kwa udhuru na pia anamdhuru.

Haifai kwake kwenda kwa familia yake pasi na sababu. Haijalishi kitu hata kama ataoa juu yake. Yeye ana haki yake na yule mwanamke mwingine ana haki yake.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (15)
  • Imechapishwa: 22/08/2020