767- Ahmad ametuhadithia: Sufyaan bin ´Uyaynah ametuhadithia, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin al-Qaasim, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa ´Aaishah ambaye amesimulia kwamba alipata ada yake ya mwezi punde tu kabla ya kufika Makkah ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia:
“Fanya kila anachofanya mwenye kuhiji.”
Ahmad amesema: Mara nyingine Sufyaan alisimulia Hadiyth namna hii:
“Fanya kila anachofanya mwenye kuhiji isipokuwa tu usitufu kwenye Nyumba.”
768- Ahmad ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa Muusa bin ´Uqbah, kutoka kwa Naafiy´, kutoka kwa Ibn ´Umar ambaye amesema:
“Anatakiwa kufanya kila anachofanya mwenye kuhiji isipokuwa tu asitufu kwenye Nyumba na kutembea kati ya Swafaa na Marwah.”
769- Ahmad ametuhadithia: ´Abdur-Razzaaq ametuhadithia, kutoka kwa Ma´mar, kutoka kwa az-Zuhriy ambaye amesema:
“Mwanamke akipata ada yake ya mwezi baada ya kutufu kwenye Nyumba, basi atembee kati ya Swafaa na Marwah wakati wa hedhi yake.”
770- Ahmad ametuhadithia: Rawh ametuhadithia: Ash´ath ametuhadithia, kutoka kwa al-Hasan aliyesema ikiwa mwanamke atapata ada yake ya mwezi baada ya kutufu katika Nyumba lakini kabla ya kuswali Rak´ah mbili nyuma ya maeneo ya Ibraahiym na kutembela kati ya Swafaa na Marwah:
“Anatakiwa kutembea. Hizo Rak´ah mbili ataziswali baada ya kutwahirika.”
- Mhusika: Imaam Abu Daawuud Sulaymaan bin al-Ash´ath as-Sijistaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ahmad, uk. 162
- Imechapishwa: 26/03/2021
767- Ahmad ametuhadithia: Sufyaan bin ´Uyaynah ametuhadithia, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin al-Qaasim, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa ´Aaishah ambaye amesimulia kwamba alipata ada yake ya mwezi punde tu kabla ya kufika Makkah ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia:
“Fanya kila anachofanya mwenye kuhiji.”
Ahmad amesema: Mara nyingine Sufyaan alisimulia Hadiyth namna hii:
“Fanya kila anachofanya mwenye kuhiji isipokuwa tu usitufu kwenye Nyumba.”
768- Ahmad ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa Muusa bin ´Uqbah, kutoka kwa Naafiy´, kutoka kwa Ibn ´Umar ambaye amesema:
“Anatakiwa kufanya kila anachofanya mwenye kuhiji isipokuwa tu asitufu kwenye Nyumba na kutembea kati ya Swafaa na Marwah.”
769- Ahmad ametuhadithia: ´Abdur-Razzaaq ametuhadithia, kutoka kwa Ma´mar, kutoka kwa az-Zuhriy ambaye amesema:
“Mwanamke akipata ada yake ya mwezi baada ya kutufu kwenye Nyumba, basi atembee kati ya Swafaa na Marwah wakati wa hedhi yake.”
770- Ahmad ametuhadithia: Rawh ametuhadithia: Ash´ath ametuhadithia, kutoka kwa al-Hasan aliyesema ikiwa mwanamke atapata ada yake ya mwezi baada ya kutufu katika Nyumba lakini kabla ya kuswali Rak´ah mbili nyuma ya maeneo ya Ibraahiym na kutembela kati ya Swafaa na Marwah:
“Anatakiwa kutembea. Hizo Rak´ah mbili ataziswali baada ya kutwahirika.”
Mhusika: Imaam Abu Daawuud Sulaymaan bin al-Ash´ath as-Sijistaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ahmad, uk. 162
Imechapishwa: 26/03/2021
https://firqatunnajia.com/ada-ya-mwezi-katika-hajj/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)