Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Uhakika wa mambo wanachotaka kusema ni kwamba utambuzi wa kumjua Allaah (´Azza wa Jall), majina na sifa Zake hautafutwi kutoka ndani ya Qur-aan, Sunnah na kwa Salaf. Badala yake kila mmoja afikirie mwenyewe; zile sifa ambazo mtu kwa kutumia akili yake anaona zinamstahikia Allaah basi amthibitishie nazo, ni mamoja zipo ndani ya Qur-aan na Sunnah au hazipo. Na zile sifa ambazo mtu kwa kutumia akili yake anaona kuwa hazimstahikii Allaah basi asimthibitishie nazo.
MAELEZO
Kwa mujibu wa maneno ya watu hawa ni kwamba yanapelekea kuwaambia watu wasichukue ´Aqiydah kutoka ndani ya Qur-aan na Sunnah, kwa sababu ndani yake hakuna ´Aqiydah sahihi na badala yake waichukue kutoka katika maneno, I´tiqaad na fikira za watu. Kwani hayo ndio sahihi. Yale yanayofahamishwa na akili na fikira zao kuhusu Allaah ndio haki na wala wasiangalie ndani ya Qur-aan, Sunnah wala maneno ya Salaf. Kwa sababu hao hawana utambuzi wa mambo hayo.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 144
- Imechapishwa: 02/09/2024
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Uhakika wa mambo wanachotaka kusema ni kwamba utambuzi wa kumjua Allaah (´Azza wa Jall), majina na sifa Zake hautafutwi kutoka ndani ya Qur-aan, Sunnah na kwa Salaf. Badala yake kila mmoja afikirie mwenyewe; zile sifa ambazo mtu kwa kutumia akili yake anaona zinamstahikia Allaah basi amthibitishie nazo, ni mamoja zipo ndani ya Qur-aan na Sunnah au hazipo. Na zile sifa ambazo mtu kwa kutumia akili yake anaona kuwa hazimstahikii Allaah basi asimthibitishie nazo.
MAELEZO
Kwa mujibu wa maneno ya watu hawa ni kwamba yanapelekea kuwaambia watu wasichukue ´Aqiydah kutoka ndani ya Qur-aan na Sunnah, kwa sababu ndani yake hakuna ´Aqiydah sahihi na badala yake waichukue kutoka katika maneno, I´tiqaad na fikira za watu. Kwani hayo ndio sahihi. Yale yanayofahamishwa na akili na fikira zao kuhusu Allaah ndio haki na wala wasiangalie ndani ya Qur-aan, Sunnah wala maneno ya Salaf. Kwa sababu hao hawana utambuzi wa mambo hayo.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 144
Imechapishwa: 02/09/2024
https://firqatunnajia.com/99-maneno-yao-yanapelekea-hivi-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)