Wakazi wa Peponi ni kila muumini na mwenye kumcha Allaah. Kwa sababu ndio wapenzi wa Allaah. Amesema (Ta´ala) kuhusu Pepo:

أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ

“Imeandaliwa kwa wenye kumcha Allaah.”[1]

أُعِدَّتْ لِلَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ 

“… imeandaliwa kwa wale waliomwamini Allaah na Mitume Yake.”[2]

Wakazi wa Moto ni kila kafiri mla maangamivu. Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu Moto:

أُعِدَّتْ لِلْكَافِرِينَ

”Umeandaliwa kwa makafiri.”[3]


فَأَمَّا الَّذِينَ شَقُوا فَفِي النَّارِ

“Ama wale walio mashakani, basi watakuwa Motoni.”[4]

[1] 03:133

[2] 57:21

[3] 02:24

[4] 11:106

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 133
  • Imechapishwa: 12/12/2022