Kuhusu uombezi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa Abu Twaalib ili awe katika adhabu ndogo ya Moto na huku amevaa viatu viwili ambavyo vinachemsha ubongo wake – na huyu ndiye mtu wa Motoni mwenye adhabu ya chini kabisa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kama isingelikuwa mimi basi angelikuwa katika tabaka la chini kabisa Motoni.”
Ameipokea Muslim.
Uombezi huu ni maalum kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kwa ami yake Abu Twaalib peke yake. Hilo – na Allaah ndiye mjuzi zaidi – ni kutokana na ile kazi aliyofanya ya kumnusuru na kumtetea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na yale aliyokuja nayo.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 130-131
- Imechapishwa: 06/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)