Ama kuwaomba msaada wafu ni jambo halijuzu kabisa. Wafu hawawezi kitu. Ni mamoja Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala mwenginewe. Wao wako katika ulimwengu na wewe uko katika ulimwengu mwingine. Kwa hiyo usitafute kutoka kwa wafu chochote kwa hoja kwamba wana karama na kwamba wana uwezo, ni batili. Maiti haombwi kitu ijapokuwa ni katika mbora kabisa wa watu.
Vivyo hivyo aliye hai haombwi asichoweza yeyote isipokuwa Allaah. Haombwi jambo la kumponya mgonjwa, kutunuku mtoto au kuleta riziki. Viumbe hawaombwi vitu asivyoweza yeyote isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-il-Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 115
- Imechapishwa: 24/05/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)