Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Dalili ya nadhiri ni Kauli Yake (Ta´ala):
يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا
“Wale ambao wanatimiza nadhiri zao na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea.”[1]
MAELEZO
Nadhiri ni kule mtu kuilazimisha nafsi yake mwenyewe kwa kitu ambacho hakikumlazimu kwa mujibu wa msingi wa Shari´ah. Kwa mfano mtu akaweka nadhiri ya kutoa swadaqah kitu fulani. Hivyo itamlazimu kutimiza nadhiri yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuweka nadhiri ya kumtii Allaah basi amtii.”[2]
Nadhiri ni aina moja wapo ya ´ibaadah isiyofaa isipokuwa kwa Allaah pekee. Mwenye kuliwekea nadhiri kaburi, sanamu au kitu kingine basi amemshirikisha Allaah. Ni nadhiri ya maasi na shirki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuweka nadhiri ya kumuasi Allaah basi asimuasi.”[3]
[1] 76:07
[2] al-Bukhaariy (6696 na 6700).
[3] al-Bukhaariy (6696 na 6700).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 154-155
- Imechapishwa: 31/12/2020
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Dalili ya nadhiri ni Kauli Yake (Ta´ala):
يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا
“Wale ambao wanatimiza nadhiri zao na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea.”[1]
MAELEZO
Nadhiri ni kule mtu kuilazimisha nafsi yake mwenyewe kwa kitu ambacho hakikumlazimu kwa mujibu wa msingi wa Shari´ah. Kwa mfano mtu akaweka nadhiri ya kutoa swadaqah kitu fulani. Hivyo itamlazimu kutimiza nadhiri yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuweka nadhiri ya kumtii Allaah basi amtii.”[2]
Nadhiri ni aina moja wapo ya ´ibaadah isiyofaa isipokuwa kwa Allaah pekee. Mwenye kuliwekea nadhiri kaburi, sanamu au kitu kingine basi amemshirikisha Allaah. Ni nadhiri ya maasi na shirki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuweka nadhiri ya kumuasi Allaah basi asimuasi.”[3]
[1] 76:07
[2] al-Bukhaariy (6696 na 6700).
[3] al-Bukhaariy (6696 na 6700).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 154-155
Imechapishwa: 31/12/2020
https://firqatunnajia.com/74-dalili-kwamba-nadhiri-ni-ibaadah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)