Ummah huu ndio wa kwanza utakaofanyiwa hesabu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Sisi ni wa mwisho na wa mwanzo wenye kutangulia siku ya Qiyaamah wataohukumiwa kabla ya viumbe wengine.”[1]
Kuna maafikiano juu yake.
Ibn Maajah amepokea kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Sisi ni Ummah wa mwisho na ni mwanzo wataofanyiwa hesabu… “[2]
Kitu cha kwanza atachofanyiwa nacho hesabu mja miongoni mwa haki za Allaah ni swalah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kitu cha kwanza atachofanyiwa nacho hesabu mja siku ya Qiyaamah ni swalah. Ikitengemaa, basi yatatengemaa matendo yake mengine, na ikiharibika, basi yataharibika matendo yake mengine.”
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw” na cheni ya wapokezi wake haina neno –Allaah akitaka. Yamesemwa na al-Mundhiriy katika “at-Targhiyb wat-Tarhiyb[3]” (01/246).
Kitu cha kwanza kitachohukumiwa kati ya watu ni umwagikaji wa damu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kitu cha kwanza kitachohukumiwa kati ya watu ni umwagikaji wa damu.”[4]
Kuna maafikiano juu yake.
[1] Muslim (856, 22) na tamko lake liko kwa al-Bukhaariy (876).
[2] Ibn Maajah (4290), Ahmad (01/282), (02/274, 342), al-Bayhaqiy katika “Dalaa-il-un-Nubuwwah” (05/482). al-Buuswiyriy amesema katika ”az-Zawaaid” (03/317):
”Cheni ya wapokezi hii ni Swahiyh na wanamme wake ni waaminifu.”
Ameisahihisha Shaykh al-Albaaniy.
[3] at-Tirmidhiy (413, an-Nasaa´iy (01/232) na Ibn Maajah (1426). Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (01/185).
[4] al-Bukhaariy (6864) na Muslim (1678, 28).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 119
- Imechapishwa: 29/11/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)