71. Uwajibu wa ile Tashahhud ya kwanza na du´aa zake zilizowekwa katika Shari´ah

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisoma Tashahhud kila baada ya Rak´ah mbili[1]. Kitu cha kwanza anachosema punde tu baada ya kukaa chini:

التحيات لله

“Maadhimisho yote yanamstahiki Allaah.”[2]

Akisahau (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Tashahhud ya kwanza, basi huleta Sujuud-us-Sahuw[3]. Aliamrisha Tashahhud na akasema:

“Mnapokaa chini kila baada ya Rak´ah mbili basi semeni:

…التحيات لله

“Maadhimisho yote yanamstahiki Allaah… “

na chagueni du´aa inayokupendezeni na mumuombe Allaah (´Azza wa Jall).”[4]

Katika upokezi mwingine imekuja:

“Semeni katika kila kitako:

…التحيات لله

“Maadhimisho yote yanamstahiki Allaah… “[5]

Vivyo hivyo alimwamrisha yule mtu aliyeswali kimakosa, kama ilivyotangulia punde tu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiwafunza Tashahhud kama anavyowafunza Suurah kutoka katika Qur-aan[6]. Sunnah ni kuisoma kimyakimya[7].

[1] Muslim  na Abu ´Awaanah.

[2] al-Bayhaqiy kupitia kwa ´Aaishah kwa cheni ya wapokezi nzuri, amesema Ibn-ul-Mulaqqin (2/28).

[3] al-Bukhaariy na Muslim. Imetajwa katika ”Irwaa’-ul-Ghaliyl” (338).

[4] an-Nasaa’iy, Ahmad na at-Twabaraaniy katika ”al-Mu´jam al-Kabiyr” (1/25/3) kwa cheni Swahiyh. Udhahiri ni kwamba imewekwa katika Shari´ah kuomba katika kila Tashahhud hata kama sio Rak´ah ya mwisho. Haya pia ndio maoni ya Ibn Hazm (Rahimahu Allaah).

[5] an-Nasaa’iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.

[6] al-Bukhaariy na Muslim.

[7] Abu Daawuud na al-Haakim ambaye ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 139
  • Imechapishwa: 30/12/2018