71 – Sulaymaan bin Harb ametuhadithia: Hammaad bin Zayd ametuhadithia, kutoka kwa Ayyuub, kutoka kwa Muhammad, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin Bishr bin Mas´uud, ambaye ameeleza:
”Kulisemwa: ”Ee Mtume wa Allaah! Umetuamrisha kukutakia amani na kukuswalia. Tumejua namna ya kukutakia amani, tunakuswalia vipi?” Akasema: ”Semeni:
اللهم صل على آل محمد، كما صليت على آل إبراهيم، و بارك على آل محمد، كما باركت على آل إبراهيم
“Ee Allaah! Wasifu jamaa zake Muhammad kama Ulivyowasifu jamaa zake Ibraahiym. Na wabariki jamaa zake Muhammad kama Ulivyowabariki jamaa zake Ibraahiym.”[1]
[1] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh lakini kuna Swahabah anayekosekana. Wanamme wote ni wanamme wa Muslim. ´Abdur-Rahmaan bin Bishr bin Mas´uud alikuwa ni Abu Bishr al-Answaariy al-Madaniy al-Azraq. Amepokea kutoka kwa Abu Mas´uud al-Answaariy, Abu Hurayrah, Abu Sa´iyd na Khabbaab al-Arat. Ibn Hibbaan amemtaja katika “ath-Thiqaat” ilihali ad-Daraqutwniy yeye amesema kwamba ”amesimulia kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pasi na Swahabah katika cheni ya wapokezi”. Kana kwamba anaashiria Hadiyth yake hii. Imepokelewa kwa cheni ya wapokezi iliyoungana kupitia kwa Abu Mas´uud al-Answaariy, lakini sio Swahiyh, kama itakavyoonekana katika ukaguzi unaofuata.
- Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 67
- Imechapishwa: 31/01/2024
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
71 – Sulaymaan bin Harb ametuhadithia: Hammaad bin Zayd ametuhadithia, kutoka kwa Ayyuub, kutoka kwa Muhammad, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin Bishr bin Mas´uud, ambaye ameeleza:
”Kulisemwa: ”Ee Mtume wa Allaah! Umetuamrisha kukutakia amani na kukuswalia. Tumejua namna ya kukutakia amani, tunakuswalia vipi?” Akasema: ”Semeni:
اللهم صل على آل محمد، كما صليت على آل إبراهيم، و بارك على آل محمد، كما باركت على آل إبراهيم
“Ee Allaah! Wasifu jamaa zake Muhammad kama Ulivyowasifu jamaa zake Ibraahiym. Na wabariki jamaa zake Muhammad kama Ulivyowabariki jamaa zake Ibraahiym.”[1]
[1] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh lakini kuna Swahabah anayekosekana. Wanamme wote ni wanamme wa Muslim. ´Abdur-Rahmaan bin Bishr bin Mas´uud alikuwa ni Abu Bishr al-Answaariy al-Madaniy al-Azraq. Amepokea kutoka kwa Abu Mas´uud al-Answaariy, Abu Hurayrah, Abu Sa´iyd na Khabbaab al-Arat. Ibn Hibbaan amemtaja katika “ath-Thiqaat” ilihali ad-Daraqutwniy yeye amesema kwamba ”amesimulia kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pasi na Swahabah katika cheni ya wapokezi”. Kana kwamba anaashiria Hadiyth yake hii. Imepokelewa kwa cheni ya wapokezi iliyoungana kupitia kwa Abu Mas´uud al-Answaariy, lakini sio Swahiyh, kama itakavyoonekana katika ukaguzi unaofuata.
Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 67
Imechapishwa: 31/01/2024
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/71-hadiyth-umetuamrisha-kukutakia-amani/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)