Kuna kidokezo muhimu maana ya maneno Yake Allaah (Ta´ala):
أَوْ نِسَائِهِنَّ
”… au wanawake wao… ”[1]
Bi maana waumini wanawake, kama alivosema Mujaahid na wengine katika Salaf, na si wanawake wema pasi na kujali dini yao, kama walivosema baadhi hii leo. ash-Shawkaaniy amesema:
”Wanawake kuegemezwa kwao kunafahamisha kuwa inawahusu waumini wa kike peke yao.”[2]
al-Bayhaqiy amesema:
”Ama kuhusu maneno Yake (Ta´ala):
أَوْ نِسَائِهِنَّ
”… au wanawake wao… ”
tumesimuliwa ya kwamba ´Umar bin al-Khattwaab alimwandikia Abu ´Ubaydah bin al-Jarraah: ”Wanawake wa Kiislamu wanaoingia bafu za nje pamoja na wanawake katika watu wa Kitabu; wazuie wasiingie.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
”Si halali kwa mwanamke anayemwamini Allaah na Siku ya mwisho, kutazama uchi wake isipokuwa watu wanaochangia imani naye.”[3]
Upokezi wa kwanza kwa al-Bayhaqiy ameupokea al-Bayhaqiy katika ”as-Sunan” kupitia kwa ´Iysaa bin Yuunus: Hishaam bin al-Ghaaz bin Rabiy´ah al-Jarshiy ametuhadithia, kutoka kwa ´Ubaadah bin Nusay al-Kindiy. Ameipokea Ibn Jariyr pia. Wapokezi wake ni wenye kuaminika, lakini cheni yake ya wapokezi imekatika kwa sababu ´Ubaadah hakuwahi kukutana na ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh). Kati yao yuko Nusay, ambaye ni baba yake na ´Ubaadah. Ibn Kathiyr ametaja katika tafsiri yake ya Qur-aan kwamba Sa´iyd bin Mansuur ameipokea katika ”as-Sunan” yake, na kupitia kwake al-Bayhaqiy: Ismaa´iyl bin ´Ayyaash ametuhadithia, kutoka kwa Hishaam bin al-Ghaaz, kutoka kwa ´Ubaadah bin Nusay, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa al-Haarith bin Qays. Wapokezi wake wote ni wenye kuaminika – isipokuwa Nusay. Hakuna mwingine isipokuwa tu Ibn Hibbaan ndiye kamzingatia kuwa ni mwenye kuaminika[4]. Haafidhw Ibn Hadjar amesema juu yake ”at-Taqriyb”:
”Hatambuliki.”
Hata hivyo wafasiri na wahakiki, kama vile Ibn Jariyr, Ibn Kathiyr, ash-Shawkaaniy na wengineo, wameafikiana juu ya maana yake. Maana yake haitoki nje ya tafsiri iliyopokelewa na haizingatii maoni ya wale waliokuja nyuma.
[1] 24:31
[2] Fath-ul-Qadiyr (4/22).
[3] Kitaab-ul-Adab, uk. 407
[4] ath-Thiqaat (5/482).
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Jilbaab-ul-Mar-ah al-Muslimah, uk. 115-116
- Imechapishwa: 09/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)