Swali 70: Wakati mwingine kipindi cha kukusanya kati ya Maghrib na ´Ishaa kwa sababu ya mvua inatokea wakafika kikosi cha watu na huku imamu anaswali ´Ishaa ambapo wakajiunga na imamu hali ya kudhani kuwa anaswali Maghrib. Ni kipi kinachowalazimu?
Jibu: Ni lazima kwao kukaa chini baada ya Rak´ah ya tatu na wasome Tashahhud na du´aa kisha watoe Tasliym pamoja naye. Baada ya hapo ndipo waswali ´Ishaa ili wapate fadhilah za mkusanyiko na kutekeleza kupangilia swalah, jambo ambalo ni lazima. Ikiwa imamu amekwishaswali Rak´ah moja basi wataswali pamoja naye Rak´ah zilizosalia kwa nia ya Maghrib na itasihi. Ikiwa imamu amekwishaswali Rak´ah zaidi basi wataswali naye zile Rak´ah walizowahi kisha watalipa zile Rak´ah zitazokuwa zimebaki. Vivyo hivyo endapo watajuwa kuwa anaswali ´Ishaa basi watajiunga pamoja naye kwa nia ya Maghrib na watafanyia kazi yale tuliyotaja halafu wataswali ´Ishaa baada ya hapo kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 73-74
- Imechapishwa: 19/09/2022
Swali 70: Wakati mwingine kipindi cha kukusanya kati ya Maghrib na ´Ishaa kwa sababu ya mvua inatokea wakafika kikosi cha watu na huku imamu anaswali ´Ishaa ambapo wakajiunga na imamu hali ya kudhani kuwa anaswali Maghrib. Ni kipi kinachowalazimu?
Jibu: Ni lazima kwao kukaa chini baada ya Rak´ah ya tatu na wasome Tashahhud na du´aa kisha watoe Tasliym pamoja naye. Baada ya hapo ndipo waswali ´Ishaa ili wapate fadhilah za mkusanyiko na kutekeleza kupangilia swalah, jambo ambalo ni lazima. Ikiwa imamu amekwishaswali Rak´ah moja basi wataswali pamoja naye Rak´ah zilizosalia kwa nia ya Maghrib na itasihi. Ikiwa imamu amekwishaswali Rak´ah zaidi basi wataswali naye zile Rak´ah walizowahi kisha watalipa zile Rak´ah zitazokuwa zimebaki. Vivyo hivyo endapo watajuwa kuwa anaswali ´Ishaa basi watajiunga pamoja naye kwa nia ya Maghrib na watafanyia kazi yale tuliyotaja halafu wataswali ´Ishaa baada ya hapo kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 73-74
Imechapishwa: 19/09/2022
https://firqatunnajia.com/70-unaposwali-maghrib-nyuma-ya-imamu-anayeswali-ishaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)