Huu ndio msimamo sahihi. Kwa msemo mwingine haijuzu kufikiria kama Khawaarij wala kufikiria kama Raafidhwah.
Khawaarij wamewakufurisha Maswahabah wengi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kama vile ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) na jeshi lake, wakawapiga vita na kuhalalisha kumwagwa damu zao.
Raafidhwah wamechupa mipaka kwa watu wa nyumbani kwake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na sambamba na hilo wakaonyesha utovu wa nidhamu kwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wengine waliosalia. Bali wamefikia mpaka kuwakufurisha, khaswa Abu Bakr na ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambao wanawaita kuwa ni “masanamu mawili ya Quraysh”. Wanawaona Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) waliafikiana juu ya dhambi na mashambulizi na kwamba walikuwa ni wanafiki, kwa sababu eti walifanya usaliti juu ya wasia wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa wasii. Raafidhwah wamesema uwongo na Khawaarij wamepotea. Allaah amewaongoza Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ambao wametambua nafasi na haki za Maswahabah. Upande mmoja hawaoni kuwa wamekingwa na makosa, upande mwingine hawaingilii yale magomvi yaliyotokea baina yao. Wanatambua kuwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) ndio ummah bora baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wanajua kuwa nafasi na ubora wao unatofautiana. Haya yametamkwa waziwazi ndani ya vitabu vya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah – Allaah avifanye kuwa wingi, awasamehe wafu wao na awanyanyue wale ambao bado wako hai ili wazidi kuwakasirisha Ahl-ul-Bid´ah kwa sampuli zao zote!
- Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Latwiyfah ´alaa Usuwl-is-Sunnah al-Muniyfah, uk. 151
- Imechapishwa: 23/06/2026
Huu ndio msimamo sahihi. Kwa msemo mwingine haijuzu kufikiria kama Khawaarij wala kufikiria kama Raafidhwah.
Khawaarij wamewakufurisha Maswahabah wengi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kama vile ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) na jeshi lake, wakawapiga vita na kuhalalisha kumwagwa damu zao.
Raafidhwah wamechupa mipaka kwa watu wa nyumbani kwake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na sambamba na hilo wakaonyesha utovu wa nidhamu kwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wengine waliosalia. Bali wamefikia mpaka kuwakufurisha, khaswa Abu Bakr na ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambao wanawaita kuwa ni “masanamu mawili ya Quraysh”. Wanawaona Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) waliafikiana juu ya dhambi na mashambulizi na kwamba walikuwa ni wanafiki, kwa sababu eti walifanya usaliti juu ya wasia wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa wasii. Raafidhwah wamesema uwongo na Khawaarij wamepotea. Allaah amewaongoza Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ambao wametambua nafasi na haki za Maswahabah. Upande mmoja hawaoni kuwa wamekingwa na makosa, upande mwingine hawaingilii yale magomvi yaliyotokea baina yao. Wanatambua kuwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) ndio ummah bora baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wanajua kuwa nafasi na ubora wao unatofautiana. Haya yametamkwa waziwazi ndani ya vitabu vya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah – Allaah avifanye kuwa wingi, awasamehe wafu wao na awanyanyue wale ambao bado wako hai ili wazidi kuwakasirisha Ahl-ul-Bid´ah kwa sampuli zao zote!
Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Latwiyfah ´alaa Usuwl-is-Sunnah al-Muniyfah, uk. 151
Imechapishwa: 23/06/2026
https://firqatunnajia.com/68-wao-si-kama-khawaarij-wala-si-kama-raafidhwah/